JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limepiga marufuku maandamano ya Waislamu yenye lengo la kupinga Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) kwa madai kuwa limewafelisha wanafunzi wa dini hiyo katika somo la elimu ya Uislamu.
BARAZA LA WAISLAMU nchini wamelilalamikia Baraza la Mitihani [NECTA] kwa kudai wanahujumiwa kwa kufelishwa kwa wanafunzi wa dini hiyo
Hayo yalibainsihwa katika mkutano uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika ukumbi wa Daimond Jubilee ambapo uliwakutanisha waislamu katika mchakato wa maoni ya katiba mpya
Baraza hilo la Waislamu lilibainisha mambo mbalimbali yanayoleta mkanganyo kwa waumini hao ikiwemo na kufelishwa kwa wanafunzi wa kiislamu na nikiwemo na hujuma inayofanyika kuhusiana na zoezi la sensa
Hivyo kufuatia hilo Baraza hilo limemtaka Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani (Necta), Dk Joyce Ndalichako kujiuzulu wadhifa huo kwa kumtuhumu kuwafelisha mitihani ya dini ya Kiislamu wanafunzi wa kidato cha sita wa dini hiyo.
Kauli hiyo ya Bakwata imetolewa na Mufti wa Tanzania, Sheikh Issa Bin Shaaban Simba katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Tanga jana kuelezea msimamo wa Waislamu nchini kuhusu matokeo ya kidato cha sita, hujuma inayoandaliwa kufanyika katika zoezi la sensa pamoja na vurugu zilizotokea Zanzibar.